Taifa letu lipo katika wakati mgumu sana ambao unahitaji maamuzi sio tu MAGUMU lakini pia MAKINI; Lakini Ugumu na Umakini huu Kimaamuzi hatuna budi kuufanya kwa kushirikiana na wananchi wa Kusini badala ya kuwabeza, lakini hasa kuingiza siasa kuliko mantiki katika kulitazama suala zima. Vinginevyo suala la ‘Resource Curse’ ambalo kwa miaka mingi tumekuwa tunalisikia tu kwa wenzetu, sasa litatukuta muda sio mrefu na wahanga watakuwa ni kila mtanzania bila ya kujalisha cheo au uwezo wa fedha; Mengi yameshajadiliwa na wadau mbalimbali kuhusiana na mgogoro huu pamoja na mapendekezo juu ya nini kifanyike ili kuokoa taifa letu lisitumbukie katika janga la ‘resource curse’; Muhimu hapa ni kuwaweka wananchi wa Kusini at the ‘Centre’ katika suala zima la gesi asilia na economic development, sio kuwaweka at the ‘Periphery’. Pia ni muhimu serikali ikatambua kwamba wananchi wa kusini wanazidi kuelimishwa kwamba faida kwao itatokana zaidi na ubora wa ‘Natural Gas Policy’, ambayo kwa bahati mbaya, tayari tunaingia katika mikataba mikubwa huku ‘Natural Gas Policy’ ikiwa katika hatua ya ‘Draft Document’; Ni masuala kama haya ndio yanachangia sana kwa serikali ‘to shoot on its own foot, na mbaya zaidi, tiba zinazotatumiwa kutibu jeraha ni tiba ambazo zinazidi kuchimba kidonda kuliko kukikausha. Ni muhimu kwa viongozi wa Serikali sasa kuja na maamuzi magumu na makini ambayo yatalenga kurudisha imani ya wananchi wa mtwara kwa serikali yao; Huu sio wakati wa siasa za ubabe na arrogance, na pia vyama vyote vya siasa ni vyema vikaliondoa suala hili majukwaani na badala yake kutafuta mazingira ya kukaa meza ya pamoja na kulifanya suala hili kuwa ‘bipartisan’ kama kweli nia ni kurudisha hali ya amani na utulivu katika taifa letu;

Leo hii, Tanzania inakadiriwa kuwa na utajiri wa gesi asilia unao karibia
43 trillion cubic feet; Hifadhi hii inakadiriwa kuwa na thamani ya dollar za kimarekani karibia Billion 450, ambayo ni sawa na karibia Shillingi trilioni 730; US geological Survey inakadiria uwepo wa hifadhi kubwa zaidi na kwamba tafiti zinazoendelea zitabainisha uwepo wa gesi wa karibia 441 trillion Cubic feet; Nyingi ya gesi hii inakadiriwa kuwepo katika maeneo ya Pwani ya Afrika mashariki, huku Tanzania ikiwa ni sehemu kubwa ya eneo hilo; Ni kwa maana hii, inakadiriwa kwamba miaka kumi ijayo, Tanzania itakuwa ni moja ya mataifa yanayozalisha gesi asilia kwa wingi Duniani; Na ni kwa mantiki hii ndio maana kampuni mbalimbali za sekta ya gesi duniani kama vile British Gas imejipanga kuwekeza Tanzania Dollar billioni 15 (kumi na tano) sawa na shillingi trilioni 24 (ishirini) na nne kwenye sekta ya gesi nchini katika kipindi cha miaka kumi ijayo; Tufahamu kwamba Dollar Bilioni Kumi na Tani ni zaidi ya nusu ya pato la sasa la nchi (GDP) ya Tanzania!!!

Migogoro yote itokanayo na rasilimali aka ‘natural resource curse’, chanzo chake huwa ni tatizo la
rent-seeking behavior na short terms gains on part of politicians and other public officials;Watanzania wanazidi kuchoka kuishi na ahadi za kisiasa majukwaani wakati wa kampeni za chaguzi kuu mbalimbali; Vinginevyo katika suala la rasilimali kama hizi (gesi), suala la faida kwa wananchi ni suala la common sense, kwani halihitaji rocket science kutambua kwamba ukosefu wa culture of transparency katika mikataba, hasa isiyoshirikisha wadau; Ndani ya dunia ya leo inayosukumwa na nguvu za utandawazi, wananchi hawahitaji kufundishwa na mtu yoyote kutambua kwamba the expected ‘revenues and investments’ from Gas, Oil, or Gold ni lazima zisaidie nchi to shift towards industrialization na kuzalisha ajira, huku pia mapato kupitia kodi yakienda kuboresha miundo mbinu, sekta za afya, elimu, na maji; Na katika haya, ni common sense kwamba wananchi wa kupewa kipaumbele ni wa vijijini, lakini hasa wale ambao wapo nyuma kimaendeleo kulinganisha na wananchi wa mikoa mingine;

Sasa inapotokea kwamba rasilimali husika inatokea maeneo yao lakini hakuna transparency katika mchakato mzima wa utilization ya rasilimali husika, migogoro lazima itajitokeza; Ni kwa mantiki hii, wananchi wa kupewa kipaumbele katika hili ni wananchi wa mikoa ya kusini ambao kwa zaidi ya miaka 50 wamekuwa hawapewi kipaumbele in terms of economic development ikilinganishwa na sehemu nyingine nyingi za nchi; Kwa maana hii, ingawa ni sahihi kusema kwamba Gesi ya Mtwara ni ya Watanzania wote, lakini pia ni sahihi kusema kwamba kwa simple logic tu ya ‘sustainability’ – kisiasa, kiuchumi, kijamii na kimazingira, faida ya gesi hii ni lazima iwe wazi kwanza pale inapotoka (source); Hivi ndivyo mataifa yaliyoendelea yalifanya; Kwa kuzingatia tu ‘simple economics’, mkoa wa Mtwara una mazingira yote muhimu yanayokidhi approach ya namna hii; kwa mfano, Mtwara tayari kuna Bandari, kuna nguvu kazi iliyo ‘idle’ ambayo kutokana na sera mbovu za serikali, nguvu kazi hiyo imegeuka kuwa wachuuzi nchi nzima, pia Mtwara ina eneo kubwa la Ardhi kwa ajili ya maendeleo ya Kilimo na Viwanda; Muhimu zaidi, Mtwara ni a better gateway kwa maendeleo ya uchumi ndani ya SADC Zone; Ni masuala kama haya ndio yanawia vigumu watu wengi kuamini kwamba ni Lazima gesi itokea kwanza Mtwara kwenda sehemu nyingine ya nchi, halafu wananchi wa mtwara waje kupata faida za gesi hii baadae; Hata simple economics zinazozingatia factors nilizojadili hapo juu zinathibitisha kwamba approach ya
is not the best alternative kiuchumi; pengine; it’s the best alternative kisiasa, hasa in the context of rent seeking behavior and short terms gains kwa wahusika;

Ebu tuujadili mkoa wa Mtwara Kidogo


Duniani kote, GDP Per Capita ni kiashiria (indicator) cha hali ya wananchi kiuchumi i.e. kipato/income. Zifuatazo ni takwimu za pato la kila Mtanzania kwa mwaka 2010 - Nimechukua kumi bora na kuziweka in ‘order of ranking’:


Jedwali la Kwanza: Vipato Vya Watanzania Kulingana na Mikoa Wanayotoka (GDP Per Capita)


MKOA PATO LA KILA MWANANCHI KWA MWAKA (T.Shillings) (2010)
1. Dar-es-salaam 1,740,947 (million)
2. Iringa 979,882 (laki)
3. Arusha 945,437
4. Mbeya 892,877
5. Kilimanjaro 879,432
6. Ruvuma 866,191
7. Mwanza 829,647
8. Tanga 763,203
9. Morogoro 744,234
10. Rukwa 726,658
Source: Bajeti Za Serikali.

Tukitizama jedwali namba moja, Mikoa ya Kusini (kama Mtwara) haipo katika orodha hii
; Je, hii ni kwa sababu gani? Pengine tutazidi elewa ndani ya mjadala wetu baadae, lakini kwa sasa tutazame takwimu nyingine:

  • Je, ni Mikoa ipi inachangia Zaidi Kwenye Pato la Taifa/Inayozalisha Bidhaa na Huduma Nyingi Zaidi Tanzania (GDP)?


Jedwali la Pili: Kumi Bora Kwa Uzalishaji Wa Bidhaa na Huduma (GDP).


MKOA UZALISHAJI WA BIDHAA NA HUDUMA (GDP) T.shillings (2010)
1. Dar-es-salaam T.sh 5.4 trillioni
2. Mwanza T.sh 3.0 trillioni
3. Mbeya T.sh 2.3 trillioni
4. Shinyanga T.sh 1.9 trillioni
5. Iringa T.sh 1.7 trillioni
6. Morogoro T.sh 1.6 trillioni
7. Arusha T.sh 1.5 trillioni
8. Kilimanjaro T.sh 1.3 trillioni
9. Kagera T.sh 1.3 trillioni
10. Ruvuma T.sh 1.2 trillioni
11. Tabora T.sh 1.2 trillioni
12. Rukwa T.sh 1.1 trillioni
Source: Bajeti Za Serikali.

Vile vile, tukitazama jedwali la pili hapo juu, mikoa ya kusini (e.g. Mtwara) pia haipo katika kumi bora katika mchango wa uzalishaji na pato la Taifa; Swali linalofuata ambalo ni la kimantiki zaidi hasa kiuchumi kuliko siasa ni je:


  • Kwanini sasa tusitumie fursa hii ya gesi asilia mikoa ya kusini kuigeuza mikoa hii na yenyewe iwe na mchango kwa pato la taifa?


Binafsim nadhani ugunduzi wa gesi ya Asilia ndio fursa pakee iliyopo ya kuifanya mikoa ya kusini nayo iwe na mchango mkubwa kwa pato la taifa kupitia uwekezaji utakaotokana na mapato ya gesi; Nasema kwamba ni fursa pekee kwa sababu kwa miaka zaidi ya hamsini, wananchi wa kusini kama nilivyokwisha jadili, wamekuwa wakipuuzwa kimaendeleo; Inaonekana kwamba sera ya serikali ni kuwekeza katika maeneo yenye michango mikubwa kwa pato la taifa (GDP contribution) na ushahidi katika hili upo kwenye takwimu juu ya vipaumbele vya bajeti kwa mikoa mbalimbali kila mwaka; Ushahidi wa hili upo katika jedwali lifuatalo:


Jedwali la tatu: Mikoa Yenye Michango Midogo Katika Uzalishaji/Pato la Taifa (bottom 5).


MKOA UZALISHAJI WA BIDHAA NA HUDUMA (GDP) T.shillings (2010)
1. Singida T.sh Billioni 661
2. Pwani T.sh Billioni 608
3. Lindi T.sh Billioni 621
4. Kigoma T.sh Billioni 906
5. Mtwara T.sh Billioni 927
Source: Bajeti Za Serikali.

Tukitazama jedwali la tatu, tunaona Mtwara, Lindi na mikoa mingine kwamba ni ya mwisho kabisa katika kuchangia pato la taifa (GDP contribution in terms of production of Goods and Services); N
ote pia Kigoma ni sehemu ya orodhahii na hatupo mbali na mgogoro mwingine mkubwa katika mkoa huu; Vinginevyo si ajabu ndio maana mikoa hii imekuwa ikitengewa fedha ndogo katika bajeti za kila mwaka kama tunavyoona kwenye jedwali namba nne hapo chini:

Jedwali la nne: Mikoa inayotengewa fedha ndogo za Bajeti (bottom five)


MKOA BAJETI YA MWAKA (T.sh) (2010)
1. Mtwara T.sh Billioni 57
2. Kigoma T.sh Billioni 56
3. Singida T.sh Billioni 50
4. Manyara T.sh Billioni 54
5. Rukwa T.sh Billioni 49
Source: Bajeti Za Serikali

Je ni mikoa gani ambayo inapewa kipaumbele katika kila bajeti? Jibu ni – Mikoa ile ile ambayo ndio inachangia kwa kiasi kikubwa pato la taifa (GDP) kama ambavyo tuliona katika jedwali namba mbili hapo juu; Mikoa hiyo pamoja na kiasi cha fedha wanazotengewa katika bajeti ni kama ifuatavyo:


Jedwali la tano: Orodha ya kumi bora – vipaumbele katika Bajeti Ya Serikali.


MKOA BAJETI YA MWAKA (T.sh)
1. Dar-es-salaam T.sh Billioni 154
2. Mwanza T.sh Billioni 135
3. Mbeya T.sh Billioni 109
4. Shinyanga T.sh Billioni 104
5. Kilimanjaro T.sh Billioni 100
6. Tanga T.sh Billioni 92
7. Kagera T.sh Billioni 88
8. Morogoro T.sh Billioni 86
9. Iringa T.sh Billioni 85
10. Arusha T.sh Billioni 81
Source: Bajeti Za Serikali


Hitimisho


Njia pekee ya ya serikali kutegua bomu lililopo ambalo linaweza pelekea nchi yetu kuingia katika machafuko yasiyokuwa ya lazima ni kwa kuzingatia hoja nilizojenga huko juu; Nimeelezea kwa hoja na takwimu juu ya jinsi gani mikoa mingi ikiwepo ya kusini mwa Tanzania imekuwa ikipuuzwa kimaendeleo kwa miaka zaidi ya hamsini kutokana na sababu moja tu kubwa -
Kutokuwa na mchango wa maana kwa pato la taifa; Kama nilivyobainisha kwa hoja na takwimu, mikoa inayopewa kipaumbele katika bajeti zetu ni ile inayochangia zaidi katika pato la taifa (GDP); Kwa mantiki hii, ni muhimu kwa Serikali kusikiliza vilio vya wananchi wa kusini ili na wao wawe sehemu ya mikoa iliyopo katika jedwali namba tano hapo juu; Vinginevyo, kama nilivyokwisha sema awali, the government is shooting on its own foot, na mbaya zaidi, its prescribing tiba ambayo sio sahihi, huku kidonda kikizidi kuchimbika; Sidhani kama serikali ina nia ya kuendelea kuzembea katika hili na kupelekea mguu kukatwa na madaktari kama njia pekee itakayobakia kutibu tatizo;