Naibu katibu
mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA Zitto Kabwe hapo jana amewaondelea
shaka wakazi wa Kigoma kwa kuwathibitishia kuwa atagombea urais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania katika uchaguzi na amewathibitishia wakazi wa Kigoma kuwa
atagombea urais katika uchaguzi mkuu mwaka 2015
Kwa mara ya
kwanza Zitto Kabwe ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Kigoma Kaskazini alitangaza
nia yake ya kugombea urais mwezi Machi mwaka huu na kuzua mjadala kwa wadau wa
siasa lakini baadhi ya wakazi wa mkoa wa Kigoma bado walikuwa hawaamini
wakidhani ni porojo za kisiasa tu
Kufuatia
shaka hiyo akiwa Kigoma Taasisi ya Meza ya Duara ilimuomba Zitto kuonana na
viongozi wa Taasisi hiyo pamoja na wananchi wengine ili kuzungumza nae kwa
lengo la kumuuliza maswali juu ya masuala mbali mbali likiwemo la yeye kugombea
urais ambapo Zitto amesisitiza nia yake
Amesema
viongozi wa kizazi kilichotangulia Umetimiza wajibu wao kwa nchi na kwamba ni
jukumu la kizazi cha sasa kuanzia pale walipoifikisha na kuisogeza nchi mbele
zaidi inapotakiwa kuwa ambapo pia ameweka wazi kuwa atagombea kupitia CHADEMA
na sio chama kingine.
Hata hivyo
Zitto Kabwe amesema si jambo la lazima kwamba liwalo na
liwe yeye kuwa rais
bali itategemea na ridhaa ya wananchi wa Tanzania.
Chanzo:Mitandao ya kijamii.
0 Maoni:
Post a Comment