Wednesday, June 27, 2012

Watanzania wengi tunalaani matukio ya Utekaji nyara Hayakubaliki.

Dr.Ulimboka alipatikana baada ya taarifa mbali mbali kusambazwa katika mitandao mbali mbali kuhusu kupotea kwake.

Dr:Steven Ulimboka
Hivi ninavyoaandika yupo ICU akiwa katika hali mbaya hajitambui.Awali katikamaelezo yake alisema kwamba walikuja watu watatu waliovalia kiraia na kujitambulisha kuwa wao ni askari. Watu hao walimchukua na kumuingiza katika gari lisilokuwa na namba na kuanza kuelekea barabara ya Bagamoyo. Huko walimfunga kitambaa usoni, kamba mikononi na miguuni kisha wakampiga huku wakimwambia amekuwa akiwasumbua kwa muda mrefu na kama wangekuwa na sindano ya sumu wangemmaliza kabisa. No comments:

0 Maoni:

Post a Comment