Friday, June 1, 2012

WABUNGE KIBAO KUMSINDIKIZA SUGU DAR LIVE


WAKATI maandalizi ya shoo bab’kubwa ya muziki wa Hip Hop iliyopewa jina la Usiku wa Sugu, yakiwa yameshakamilika, wabunge kibao, bila kujali itikadi za vyama vyao wameahidi kujitokeza kumsindikiza mbunge mwenzao, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ atakayeongoza shoo hiyo ndani ya Ukumbi wa Dar Live, Mbagala Zakhem.
Akizungumza na Ijumaa kwa njia ya simu kutokea nchini Switzerland alikoenda kujifua sambamba na kufuatilia fursa za maendeleo kwa wananchi wake, Sugu atakayekamua na Profesa Jay na Juma Nature, aliwataja wabunge watakaomsindikiza Jumapili hii (Juni 3, 2012) kuwa ni Ester Bulaya, Idd Azzan, Amos Makala ambaye pia ni Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Zitto Kabwe, Freeman Mbowe, John Mnyika na wengine wengi.
“Tumeamua kumsindikiza Sugu katika shoo ya Dar Live bila kujali itikadi zetu kwa sababu anatuwakilisha wabunge wote. Kizuri zaidi kilichotufurahisha ni kwamba mapato yatakayopatikana ameahidi kuyatumia kutunisha mfuko wa elimu jimboni Mbeya.
“Tunaamini wanafunzi walioshindwa kuendelea na masomo kutokana na ukosefu wa karo, watalipiwa na shoo ya Usiku wa Sugu, kwa kweli ametufurahisha sana, lazima tumuunge mkono Jumapili hii,” alisema mbunge mmoja wa chama tawala kwa sharti la kutochapisha jina lake gazetini.

Globalpublishers

1 comment:

  1. Inapembeza sana nadhani huu ni mwanzo mzuri wa kushirikiana bila kujali itikadi

    ReplyDelete