Mkutano muhimu wa kilele kuhusu mustakbal wa Umoja wa Ulaya unalenga 
kuweka kando masilahi ya kitaifa,na kuafikiana kuhusu bajeti ya 
kugharimia miradi ya kubuni nafasi zaidi za kazi hadi ifikapo mwaka 2020
"Ulaya yenye nguvu bila ya kulazimika kutoa pesa zaidi":huo ndio msimamo
 ambao Ujerumani inatapanga kuutetea katika mazungumzo ya kubuni bajeti 
ya muda mrefu ya Umoja wa Ulaya.Pale viongozi wa taifa na serikali wa 
mataifa 27 watakapokutana kuanzia leo alkhamisi hadi kesho ijumaa mjini 
Brussels,serikali kuu ya Ujerumani inataka kuona gharama zote za Umoja 
wa Ulaya katika kipindi cha mwaka 2014 hadi 2020 zinaambatana ipasavyo 
na mahitaji halisi.Matumizi bora ndio kauli mbiu ambayo kwa kansela 
Angela Merkel haimaanishi chengine isipokuwa kupunguzwa bajeti ya Ulaya 
ya mabilioni ya Euro.
Ujerumani inachangia moja kwa tano ya bajeti jumla ya Umoja wa Ulaya 
kiwango ambacho kinafikia Euro bilioni 200 ikizingatiwa bajeti ya 
kuanzia mwaka 2007 hadi mwaka huu wa 2013.Wakati wa mkutano pamoja na 
waziri mkuu wa Italy Mario Monti hapo awali mjini Berlin,kansela Angela 
Merkel alikumbusha kwamba"Ujerumani ni mojawapo ya wachangiaji wakubwa 
miongoni mwa nchi za Umoja wa Ulaya,Na hiyo ndio maana wanapendelea 
kuona kwamba fedha zinatumiwa kwa namna ambayo zitachangia ipasavyo 
kuufanya Umoja wa Ulaya uzidishe bidii na kuwa uwanja muhimu wa 
mashindano ya kibiashara."
Upinzani wa nchi za kusini mwa ulaya
Hata alipokutana na waziri mkuu wa Hispania Mariano Rajoy na rais 
Francois Hollande wa Ufaransa,hakuchelea kansela kutilia mkazo madai ya 
Ujerumani,siku chache kabla ya mkutano huo wa kilele kuanza.
Sambamba na kupunguza nakisi,kanasela Angela Merkel anataka pia matumizi
 katika bajeti ya pamoja ya Umoja wa Ulaya yawekewe kikomo.
"Matumizi ya Umoja wa Ulaya yanabidi yasiruhusiwe kupindukia asili mia 
moja ya pato la kijamii katika Umoja wa Ulaya-amesema mchambuzi wa 
masuala ya fedha wa Umoja wa Ulaya Friedrich Heinemann wa taasisi ya 
uchunguzi wa kiuchumi ya mjini Mannheim.Inamaanisha kwamba bajeti ya 
Umoja wa Ulaya iongezeke tu ikiwa shughuli za kiuchumi za nchi za Umoja 
huo zitanawiri na kwa namna hiyo kuongezeka pia pato la ndani la kila 
mkaazi wa Umoja wa ulaya.
Nchi nyingi za Umoja wa Ulaya,ikiwa ni pamoja na 
Austria,Finland,Itali,Uholanzi na Sweden zinauunga msimamo wa 
Ujerumani.Lakini nchi zinazopokea misaada mfano wa 
Uhispania,Ureno,Ugiriki na nyengine zinaupinga.
Ajira ya vijana ndio kipa umbele
Ujerumani inataka kuona fedha nyingi zaidi zikitolewa kugharimia miundo 
mbinu ya nishati na miradi ya uchunguzi barani Ulaya.Halmashauri kuu ya 
Umoja wa Ulaya inapendekeza Euro bilioni 120 kwaajili ya miradi 
hiyo.Katika bajeti ya mwaka 2007 hadi mwaka huu wa 2017 asili mia 80 ya 
bajeti ya Umoja wa Ulaya ilikuwa ikitumika kusaidia shughuli za kilimo 
na miradi mengine ya kimkoa.Ujerumani ingependelea kuona fedha za 
kughamiria miradi ya kilimo na kimkoa zinafutwa.Katika wakati ambapo 
Ufaransa inataka kuona fedha hizo zinaendelea kutolewa Ujerumani inataka
 kuona zinatumika kupambana na ukosefu kazi miongoni mwa vijana.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

0 Maoni:
Post a Comment